Mike Sonko ni mwanasiasa maarufu nchini Kenya kwa kuwa na muonekano wa kiujana zaidi au unaweza kusema ni kisharobaro ziadi. Sonko anapenda kupendeza kwa kuvaa kofia,vito vya thamani,T shirts za kisasa,jeans na wakati mwingine kupaka rangi nywere zake....>>>>
Nyakati tofauti seneta huyu amehusishwa kwenye vituko mbalimbali, hivi sasa kituko chake kilicho-make headline ni pale alipomuweka Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta loudspeaker mbele za watu.
Kwenye moja ya mahojiano na kituo cha television Mike Sonko alisema kwamba alifanya hivyo ili waandishi wa habari wasikie kauli ya kiongozi wa nchi. Tukio lililokua linatokea hapo ni kanisa moja lilikuwa linabomolewa na Sonko hakukubaliana na hilo swala, akaamua kutafuta usaidizi kwenye ngazi za juu.
Video yenyewe ndio hii na mwisho wa siku Sonko alifanikiwa kusimamisha hiyo bomoa bomoa.
0 comments:
Post a Comment