Kiongozi wa genge kubwa la wauza madawa ya kulevya Servando Gomez alikamatwa katika oparesheni iliyotekelezwa katika jimbo la Michoacan nchini Mexico hapo jana.
Kiongozi huyu wa kundi lililowahangaisha wananchi wa Mexico alikuwa mlengwa wa kwanza wa jitihada za Rais Enrique Pena Nieto za kupambana na wauzaji wa madawa ya kulevya nchini humo.
Serikali ilikuwa imeahidi zawadi ya dola milioni 2 kwa mtu ambaye angesaidia kukamatwa kwa kiongozi huyo.
Kabla ya kujiingiza katika biashara ya madawa ya kulevya Servando Gomez alikuwa mwalimu wa shule ya msingi.
Gomez atafikishwa mahakamani kujibu jumla ya mashtaka 8 yanayomkabili.
0 comments:
Post a Comment