Leo katika historia Jumanne, Machi 10, 2015

Leo ni Jumanne tarehe 19 Jamadil Awwal 1436 Hijria sawa na Machi 10, 2015.
Siku kama ya leo miaka 525 iliyopita Abulfadhl Abdulrahman Suyuti, mashuhuri kwa lakabu ya Jalaluddin, faqihi, mpokezi wa hadithi na mtaalamu maarufu wa lugha wa zama hizo alifariki dunia mjini Cairo. Jalaluddin Suyuti alizaliwa mwaka 849 Hijria na alihifadhi Qur'ani Tukufu akiwa kijana. Jalaluddin Suyuti kwa miaka kadhaa alijifunza masomo ya fiqih, hadithi, tafsiri ya Qur'ani na lugha na kupata mafanikio makubwa. Msomi huyo wa Cairo ameandika vitabu vingi vya thamani na miongoni mwavyo ni "Al Iqtirah", "Al Kitabul Kabir" na "Tarikhul Khulafaa".
Tarehe 10 Machi miaka 139 iliyopita mvumbuzi wa Kimarekani Alexander Graham Bell alivumbua simu na siku hiyo hiyo akafanya mazungumzo ya kwanza ya majaribio ya simu na msaidizi wake Thomas Watson. Uvumbuzi huo wa simu ulileta mabadiliko makubwa katika vyombo vya mawasiliano.
Bell alifaidika na uzoefu na majaribio ya wahakiki na wavumbizi wengine katika kutengeneza chombo hicho cha mawasiliano ya haraka.
Baada ya hapo chombo cha simu kiliboreshwa na kufikia kiwango cha sasa kwa kukamilishwa kazi iliyofanywa na Alexander Graham Bell.
Tarehe 10 Machi siku kama ya leo miaka 119 iliyopita jeshi la Italia lilishindwa vibaya katika jaribio lake la kutaka kuivamia na kuikalia kwa amabavu Uhabeshi au Ethiopia ya sasa. Lengo kuu la shambulizi hilo la Italia lilikuwa ni kuiungunisha Ethiopia na makoloni mengine mawili ya nchi hiyo yaani Somalia na Eritrea. Katika vita hivyo jeshi la Italia lilipata kipigo na hasara kubwa ya hali na mali licha ya kuwa na silaha za kisasa na kulazimika kurudi nyuma.
Na siku kama ya leo miaka 70 iliyopita wakati wa Vita vya Pili vya Dunia ndege za kivita za Marekani zilifanya mashambulizi makubwa dhidi ya mji mkuu wa Japan, Tokyo. Mashambulizi hayo makubwa yalishirikisha mamia ya ndege kubwa za kurusha mabomu za Marekani zilizomimina mabomu kwa mara kadhaa katika mji mkuu wa Japan. Karibu raia laki moja wa nchi hiyo waliuawa katika mashambulizi hayo.
Share on Google Plus

About nellychazzy

I Run And Own Nellychazy.blogspot.com. Working With Web Editing, Blogs Template Fix And Editing (HTML). Monitoring click4hosting.net Deals with Web hosting. Also Base On Software And Hardware, Phones,Computer
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Blogger Tricks