Waziri wa Mambo ya Nje wa utawala wa Israel ametaka Waarabu wote
wanaoishi katika ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu wakatwe
vichwa.
Avigdor Lieberman alisema hivyo jana kuwa, inabidi vichwa vya Waarabu
wote wanaoishi katika ardhi za Palestina kwa mabavu vitenganishwe na
miili yao.
Waziri huyo mwenye misimamo mikali amesema: “… kila anayetupinga
hapaswi kupewa fursa yoyote ya kuishi lazima tuchukue shoka na kuwakata
vichwa vyao vinginevyo hatutaweza kukaa salama hapa.” Mwanasiasa huyo
kutoka chama chenye misimamo mikali cha Yisrael Beytenu amesema hayo
katika kampeni za uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika katikati ya mwezi
huu.
Mara kwa mara Lieberman amekuwa akitoa maneno yaliyojaa chuki dhidi
ya Waarabu akiwaita kuwa wote ni magaidi na kutaka kutolewa hukumu za
kifo kwa kila Mwarabu anayepinga siasa za Israel.
Amewahi pia kuutaka utawala wa Israel uwashambulie kwa mabomu ya nyuklia Waislamu wa Palestina wanaishi katika Ukanda wa Ghaza.
- Blogger Comment
- Facebook Comment
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)
0 comments:
Post a Comment