Arsenal yafufua matumaini mapya UEFA, baada ya kuikalisha Bayern Munich


Picha ikionyesha matukio mbalimbali katika mchezo huo yaliyozaa magoli kwa upande wa Arsenal.
Picha ikionyesha matukio mbalimbali katika mchezo huo yaliyozaa magoli  mawili kwa upande wa Arsenal.
Klabu ya Arsenal FC wamefanikiwa kuibuka na ushindi wa kwanza kwenye michuano ya klabu bingwa barani Ulaya kwa kutibua rekodi ya Bayern Munich kwa kuifunga kwa goli 2-0 kwenye dimba la Emirates, London usiku wa Jumanne.
Kabla ya mchezo dhidi ya Arsenal, Bayern ilikuwa haijapoteza hata mchezo mmoja kati ya michezo 12 iliyokuwa imecheza msimu huu kwenye mashindano yote huku ikiwa imefunga jumla ya magoli 40.
Olivier Giroud akishangilia baada ya kuifungia Arsenal bao la kwanza
Olivier Giroud akishangilia baada ya kuifungia Arsenal bao la kwanza
Olivier Giroud alianza kuifungia Arsenal goli la kwanza dakika ya 77 ikiwa ni dakika tatu tu tangu aingie kuchukua nafasi ya Theo Walcott aliyepumzishwa kumpisha nyota huyo wa timu ya taifa ya Ufaransa.
Giroud alifunga goli hilo akiunganisha mpira wa adhabu ndogo uliopigwa na Santi Cazorla.
Mesut Ozil akiifungia Arsenal bao la pili.
Mesut Ozil akiifungia Arsenal bao la pili.
Mesut Ozil iliihakikishia Arsenal pointi tatu baada ya kufunga goli la pili dakika ya 90 ya mchezo huo baada ya kupokea pasi kutoka kwa Hector Bellerin.
Mchezo huo unakuwa ni wa kwanza kupoteza msimu huu kwa upande wa The Bavarians wakati ushindi huo kwa Arsenal ni wa kwanza kwenye michuano hiyo kwenye msimu huu.
Licha ya kutawala mchezo mchezo huo kwa asilimia nyingi, bado haikutosha kwa wakali hao wa Bundesliga kutoka Ujerumani kuchukua pointi tatu mbele ya Arsenal.
Matokeo hayo yanaifanya Arsenal kukusanya paointi tatu za kwanza kwenye michuano hiyo na kujikita nafasi ya tatu huku Bayern wakiwa kileleni mwa kundi F kwa kuwa na pointi sita sawa na Olympiacos lakini wakitofautiana wastani wa magoli ya kufunga na kufungwa.
Arsenal ina pointi sawa na Dinamo Zagreb (pointi tatu) lakini The Gunners wanakaa juu kwa wastani mzuri wa magoli ya kufunga na kufungwa.
Matokeo ya mechi nyingine zilizopigwa jana usiku ni kama ifuatavyo:
Matokeo ya mechi za UEFA Jumanne usiku.
Matokeo ya mechi za UEFA Jumanne usiku.
Share on Google Plus

About nellychazzy

I Run And Own Nellychazy.blogspot.com. Working With Web Editing, Blogs Template Fix And Editing (HTML). Monitoring click4hosting.net Deals with Web hosting. Also Base On Software And Hardware, Phones,Computer
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Blogger Tricks