Fifa wameondoa adhabu ya siku 90 za kutojishughulisha na michezo iliyokuwa imewekwa dhidi ya gwiji wa Ujerumani Franz Beckenbauer....>>>
Beckenbauer, mshindi wa Kombe la Dunia akiwa kama kocha na nahodha, siku ya Ijumaa aliambiwa kuwa adhabu hiyo imondolewa haraka iwezekanavyo, alisema meneja Marcus Hoefl.
Franz, 68, alisimamishwa baada ya kushindwa kusaidia uchunguzi wa tuhuma za rushwa kwa wagombea uwenyeji wa Kombe a Dunia 2018 (Urusi) na 2022 (Qatar).
Alikuwa sehemu ya kamati kuu ya Fifa ambao walitoa tuzo hizo.
Beckenbauer alinyanyua Kombe la Dunia kama mchezaji (1974) na kocha (1990).
0 comments:
Post a Comment