Hii ni kali nyingine kutoka Kenya,Cheki ugumu wa sheria hii mpya inayotaka kuundwa.

Kenya's Supreme Court judges file into the chamber during the opening of the 11th Parliament in NairobiSheria mpya inatengenezwa Kenya sheria hiyo itawataka wanaowazungumzia wakuu wa serikali kufanya mazoezi ya kutosha,kwani sheria hii ikipitishwa basi inamaana kwamba Rais,Naibu wake na wake zao pekee ndiyo watakao pewa jina Mtukufu au His/Her Excellency..>>>


 Unaambiwa yeyote atakaye kosa kuzingatia hilo adhabu yake atafungwa mwaka mmoja Gerezani au kutozwa faini ya shilingi milioni moja pesa za Kenya sawa na dola elfu 12 za Marekani.
 Yeyote atakaye vunja sheria ya kukosa kumuita Mbunge kwenye bunge la kitaifa Mheshimiwa au Honorable atafungwa mwaka mmoja au faini ya shilingi milioni mbili pesa za Kenya.
 Kwenye mpangilio Rasmi wa Itifaki ama pecking order Rais atafatiwa na Naibu wake kisha Spiker wa bunge la taifa,Jaji mkuu,Seneta,Mbunge wa Jimbo na wa mwisho ni Gavana.
 Sheria hiyo pia inapendekeza kwamba spika wa bunge la taifa kuitwa Right honourable ama Mheshimiwa mkuu na Jaji mkuu kuitwa his/herloadship,itakua kosa vile vile kumuita mwakilishi wa Jimbo Mheshimiwa hilo ni jina la Mbunge wa Bunge la Taifa peke yake.
 Muswada huo uliotungwa na kuwasilishwa Bungeni na Mbunge Mheshimiwa Aden keynan anaye sema kwamba sheria hiyo itasaidia kutoa mpangilio wa vyeo kwa Taifa pia anapendekeza kwamba watumishi wa umma watakao jilimbikizia vyeo watatozwa faini ya Dola milioni mbili.
 Mswada huo unajadiliwa Bungeni wakati magavana serikali ya kitaifa, wabunge na mahakama wako kwenye vita vya kubaini ni nani anauwezo wa kutekeleza majukumu na mamlaka ya kutoa muelekeo kwenye maswala mbali mbali yanayo husu usimamizi.
Share on Google Plus

About nellychazzy

I Run And Own Nellychazy.blogspot.com. Working With Web Editing, Blogs Template Fix And Editing (HTML). Monitoring click4hosting.net Deals with Web hosting. Also Base On Software And Hardware, Phones,Computer
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Blogger Tricks