Muimbaji kufungwa jela kwa kutaka kumuua Rais Kagame


Mwanamuziki wa Rwanda Kizito Mihigo
Mwanamuziki wa Rwanda Kizito Mihigo
Muimbaji maarufu wa Rwanda amehukumiwa kifungo cha miaka 10 jela baada ya kushtakiwa kwa njama za kutaka kumuua Rais Kagame na kuonyesha chuki dhidi ya serikali.
Kizito Mihigo awali alisema alikuwa na makosa na kuomba msamaha, akimaanisha hukumu yake ipunguzwe.
Kizito Mihigo amekuhumiwa jela miaka 10 kwa njama za kutaka kumuua Rais Paul Kagame
Kizito Mihigo amekuhumiwa jela miaka 10 kwa njama za kutaka kumuua Rais Paul Kagame
Mshtakiwa mwenzake, Cassien Ntamuhanga kiongozi wa kituo cha redio ya Kikristo, alifungwa miaka 25 kwa ugaidi na matusi.
Ameendelea kukataa mashtaka yote.
Rais wa Rwanda Paul Kagame
Rais wa Rwanda Paul Kagame
Mihigo alikubali kutumiana ujumbe na kundi la upinzani lenye maskani Afrika Kusini, Rwanda National Congress (RNC).
Alifutiwa mashtaka ya ugaidi huku Ntamuhanga alifutiwa kosa la kupanga kumuua Rais Kagame.
Share on Google Plus

About nellychazzy

I Run And Own Nellychazy.blogspot.com. Working With Web Editing, Blogs Template Fix And Editing (HTML). Monitoring click4hosting.net Deals with Web hosting. Also Base On Software And Hardware, Phones,Computer
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Blogger Tricks