Arsenal yamtolea macho Marco Reus

Arsenal watamgeukia Marco Reus endapo Walcott ataondoka msimu huu
Arsenal watamgeukia Marco Reus endapo Walcott ataondoka msimu huu
Arsenal inamtolea macho nyota wa Borussia Dortmund Marco Reus kuchukua nafasi ya Theo Walcott.
Winga wa Uingereza alianza kumuudhi Arsene Wenger kwa kudai mazungumzo ya mkataba mpya bado hayajaanza, pamoja na kwamba kocha huyo wa Washika Bunduki amerudia kuzungumza kinyume.
Arsenal washaanza kutafuta mrithi wa Theo Walcott ambaye mkataba wake unakaribia kumalizika
Arsenal washaanza kutafuta mrithi wa Theo Walcott ambaye mkataba wake unakaribia kumalizika
Wenger alithibitisha lengo la klabu hiyo kumpa mkataba mpya Walcott tangu Februari na alipoulizwa kuwa mazungumzo yalianza Machi 13, kocha huyo alijibu: “Mazungumzo ya kwanza yalishafanyika na tutaona yatakavyoendelea.”
Hata hivyo, Walcott, ambaye kwa sasa analipwa pauni 90,000 kwa wiki, aliandika kwenye Twitter kumchanganya kocha wake.
Walcott amerudi kutoka majeruhi na anapambana kurudi kwenye kikosi cha kwanza
Walcott amerudi kutoka majeruhi na anapambana kurudi kwenye kikosi cha kwanza
Nyota huyo 26, anataka mshahara wa pauni 100,000 kwa wiki kusaini mkataba mpya kwenye Uwanja wa Emirates.
Akiwa hana uhakika kucheza kikosi cha kwanza, pia uongozi wa Arsenal unaonekana kukataa kufikia mahitaji ya Walcott.
Marco Reus, ambaye aliifungia Ujerumani dhidi ya Australia, amekuwa akimvutia kocha Arsene Wenger
Marco Reus, ambaye aliifungia Ujerumani dhidi ya Australia, amekuwa akimvutia kocha Arsene Wenger
Vilevile, Walcott anaonekana kuchangikiwa kwa kukosa mechi baada ya kurudi kutoka kwenye majeraha ya goti ya muda mrefu.

Share on Google Plus

About nellychazzy

I Run And Own Nellychazy.blogspot.com. Working With Web Editing, Blogs Template Fix And Editing (HTML). Monitoring click4hosting.net Deals with Web hosting. Also Base On Software And Hardware, Phones,Computer
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Blogger Tricks