Aliyekuwa mbunge wa Kigoma Kaskazini Zitto Zubeir Kabwe ameliandikia barua bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutangaza kung’atuka katika bunge hilo.
Zitto ambaye alikuwa mbunge kupitia tiketi ya Chama cha Demokrasia alifanya maamuzi hayo baada ya kuvuliwa uanachama wake mapema mwezi Machi.
Mbunge huyo machachari amemaliza sintofahamu za wananchi pamoja na bunge hasa baada ya Spika wa Bunge kusema kuwa hatambui kuvuliwa kwa ubunge wake wakati walipoanza vikao vya bunge Machi 17, 2015.
Kwa sasa msomi huyo wa uchumi ambaye alisema hagombei tena ubunge anatarajiwa kuhamia chama cha ACT (Alliance for Change and Transparency) kinachotarajiwa kuzinduliwa rasmi Machi 29, 2015.
0 comments:
Post a Comment