Kijana huyo, 12, alifariki Jumapili “baada ya kupigwa na mwalimu siku iliyopita”, ilisema taarifa ya wizara.
Taarifa hiyo ilisema mwalimu huyo amefukuzwa na “uchunguzi wa kina” umeanza kufuatia mazingira ya kifo cha mtoto.
Mtoto huyo alikuwa na majeraha ya kichwani na alipatwa na matatizo ya ubongo, mchunguzi wa idara ya vifo Hisham Abdel Hamid aliiambia AFP.
Adhabu ni jambo la kawaida katika shule za Misri, ambapo uzembe umetajwa kutokana na vifo vya watoto wawili mwishoni mwa 2014 kutokana na matumizi mabaya ya vifaa.
Idadi ya kuwanyanyasa watoto imefikia hatua ya hatari.
0 comments:
Post a Comment