Ronaldo apiga bao 5 wakati Madrid ikiibuka na ushindi mkubwa

Ronaldo akishangilia bao
Ronaldo akishangilia bao
Kikosi cha Madrid kikiwa nyumbani kimefanikiwa kuibuka na ushindi wa mabao 9-1 dhidi ya Granada katika mchezo wa ligi kuu ya Hispania La Liga.
Ronaldo akituliza mpira kifuani
Ronaldo akituliza mpira kifuani
Ushindi wa Madrid umepatika kupita kwa wachezaji Cristiano Ronaldo mabao matano katika dakika ya ( 30, 36, 38, 54, 91 ), Karim Benzema mabao mawili katika dakika ya ( 52, 56 ) na bao moja kupitia kwa Gareth Bale katika dakika ya 25.
Ronaldo akiwapita walinzi wa timu ya Granada
Ronaldo akiwapita walinzi wa timu ya Granada
Kwa ushindi huo Madrid imerudi kwenye mbio za kupigania ubingwa wa ligi kuu ya La liga huku ikitoa salamu kwa washindani wake kuwa wao hawajakata tamaa ya kupigania ubingwa huo.
wachezaji wa Madrid wakishangilia baada ya bale kufunga bao la kwanza
wachezaji wa Madrid wakishangilia baada ya bale kufunga bao la kwanza
Upande wa rekodi  unaonesha kuwa mara ya mwisho Granada kuifunga Madrid ilikuwa ni mwaka 1974 ambapo iliibuka na ushindi wa bao 1-0.
James akipiga shuti kuelekea kwenye lango la Granada
James akipiga shuti kuelekea kwenye lango la Granada
Kikosi cha Madrid ni: Casillas, Arbeloa, Varane, Ramos, Marcelo, Modric, Kroos, James, Bale, Benzema, Ronaldo
Benchi : Navas, Coentrao, Nacho, Illarramendi, Lucas Silva, Jese, Chicharito.
Kikosi cha Granada: Oier; Foulquier, Babin, Mainz, Juan Carlos; Fran Rico, Iturra; Ibanez, Rochina, Candeias; El-Arabi.
Benchi : Nyom, Javi Marquez, Piti, Riki, Roberto, Eddy, Murillo.
Share on Google Plus

About nellychazzy

I Run And Own Nellychazy.blogspot.com. Working With Web Editing, Blogs Template Fix And Editing (HTML). Monitoring click4hosting.net Deals with Web hosting. Also Base On Software And Hardware, Phones,Computer
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Blogger Tricks