Snoop Dogg amebainisha kuwa alikuwa amevuta (bangi) wakati alipokutana na Rais Barack Obama, na hata kuingia katika bafu la White House na kuvuta tena.
Rapa huyo mkongwe, 43, aliulizwa na Andy Cohen kwenye kipindi cha Watch What Happens Live kuhusu tabia yake ya uvutaji wakati alipoulizwa kuhusu tukio kubwa alilowahi kulifanya.
“Ikulu ya Marekani,” alijibu. “Lilikuwa jambo maridhawa. Tukio la miaka.”
Pia alidai angependa kukutana na Rais baada ya kumaliza muda wake mwakani ili wazungumze vizuri.
“Nataka nikutane naye akitoka ofisini ili tuzungumze hasa kilichotokea,” alitabasamu.
Na alipoulizwa kama aliingia bafuni kwa ajili ya kuvuta tena, alisema; “Huko ndiko nlikojaribu kuingia, unanisoma? Nikakutana na mlinzi na nikapishana naye kiaina aina.”
0 comments:
Post a Comment