Mourinho ‘alikoroga’ tena


Moja kati ya madhambi yaliyokuwa yakifanywa na wachezaji wa Dynamo Kiev dhidi ya wachezaji wa Chelsea
Moja kati ya madhambi yaliyokuwa yakifanywa na wachezaji wa Dynamo Kiev dhidi ya wachezaji wa Chelsea
Kocha wa klabu ya Chelsea, Jose Mourinho, amejiweka tena matatani kwa kumtolea lugha ya kashfa muamuzi, Damir Skomina, aliyechezesha mechi yao ya ligi ya mabingwa barani Ulaya  dhidi Dynamo Kiev ambapo mechi iliishia kwa sare ya bila kufungana.

Fabregas (kulia) akiongea na muamuzi akihoji ni kwanini amenyimwa penati ya wazi
Fabregas (kulia) akiongea na muamuzi, Damir Skomina,  (kushoto)  akihoji ni kwanini amenyimwa penati ya wazi.
Mourinho alimuita muamuzi huyo kama mtu dhaifu na asiyekuwa na maamuzi ya busara, baada ya kuinyima timu yake penati ya wazi baada ya kiungo Cesc Fabregas kufanyiwa madhambi eneo la penati.
Maneno hayo yanaweza kumletea matatizo kocha huyo na ikumbukwe kuwa ni siku chache tuu zimepita tangu Mourinho atozwe faini ya pauni elfu 50 na chama cha soka nchini Uingereza (FA) kwa kumtolea lugha chafu mwamuzi, Robert Madeley.
Share on Google Plus

About nellychazzy

I Run And Own Nellychazy.blogspot.com. Working With Web Editing, Blogs Template Fix And Editing (HTML). Monitoring click4hosting.net Deals with Web hosting. Also Base On Software And Hardware, Phones,Computer
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Blogger Tricks