Obama akaribia kumfunika Justin Bieber kwenye YouTube kupitia kipindi chenye maswali ya kejeli.

Obama akaribia kumfunika Justin Bieber kwenye YouTube kupitia kipindi chenye maswali ya kejeli

Rais Barack Obama wa Marekani ambaye hupenda kujichanganya mara kwa mara na kuonesha jinsi anavyotaka kuwafikia watu aina zote, hivi karibuni alifanya mahojiano na Zach Galfianakis katika kipindi cha ‘Between Two Ferns’ kinachowekwa kwenye mtandao.

Kipindi hicho ambacho huwa na maswali mengi ya kejeli na ya kukwaza wakati mwingine, huwekwa kwenye tovuti ya Funny or Die.
Tovuti hiyo imeeleza mwishoni mwa wiki kuwa kipindi alichofanya Zach Galfianakis na Barack Obama na kuwekwa kwenye akaunti yao ya YouTube kimeangaliwa zaidi ya mara milioni 15 na hivyo kinaonesha dalili ya kuwa kitavunja rekodi ya mahojiano na Justin Bieber ambaye kipindi chake kilifikisha viewers milioni 17.8.
Baada ya kufanya mahojiano na kipindi hicho na kutupiwa maswali kadhaa ya kejeli, Ijumaa ya wiki iliyopita Obama alimwambia Ryan Seacrest katika mahojiano kuwa kwa kufanya vile anaamni ameweza kuwafikia vijana wengi na ujumbe wa sera yake ambapo hata binti yake Malia alikuwa amevutiwa baada ya kusikia kuwa amerekodi kipindi na Galfianakis.
Obama alipata nafasi ya kuzungumza kuhusu sera yake ingawa asilimia 97 ya mahojiano ilijaa kejeli na maswali ya ucheshi.
Share on Google Plus

About nellychazzy

I Run And Own Nellychazy.blogspot.com. Working With Web Editing, Blogs Template Fix And Editing (HTML). Monitoring click4hosting.net Deals with Web hosting. Also Base On Software And Hardware, Phones,Computer
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Blogger Tricks