Sasa ni Nifasi kwa Wanawake:: Mwanamke kuwa kocha mkuu Ufaransa


Helena Costa amewahi kuwa kocha wa timu za wanawake nchini Iraq na Qatar
Klabu ya soka ya Ufaransa iliyo katika ligi ya daraja ya pili, Clermont,imemteua mwanamke raia wa Portugal Helena Costa kama kocha wake mkuu.
Uteuzi huu unamfanya mwanamke huyo kuwa wa kwanza kuwahi kushikilia wadhifa wa juu zaidi wa umeneja kama huu katika soka ya wanaume barani Ulaya....>>>>>

Klabu hiyo kwa jina, Clermont, ilisema kuwa kocha mpya Helena Costa, aliyekuwa kocha wa timu za taifa za wanawake nchini Qatar na Iraq, ataanza kazi msimu ujao.
Costa pia aliwahi kuwa afisa wa klabu ya Celtic nchini Scotland ambaye kazi yake ilikuwa kuwatafuta wachezaji chipukizi wenye kipajii cha juu kuchezea klabu hiyo.
Pia aliwahi kuwa kocha wa timu ya wanawake ya Iran tangu mwaka 2012.
Klabu ya Clermont imesema kuwa ina matumaini makubwa kwamba Helena atasaidia klabu kupiga hatua.
Atachukua nafasi ya Regis Brouard, ambaye mkataba wake unakamilika mwishoni mwa msimu.

Klabu hiyo inashikilia nafasi ya 14 katika ligi ya daraja ya pili.
Share on Google Plus

About nellychazzy

I Run And Own Nellychazy.blogspot.com. Working With Web Editing, Blogs Template Fix And Editing (HTML). Monitoring click4hosting.net Deals with Web hosting. Also Base On Software And Hardware, Phones,Computer
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Blogger Tricks