Katibu Mkuu wa Fifa Jerome Valcke amesema Kombe la Mataifa Afrika 2023 litaahirishwa kutoka Januari hadi Juni kusaidia kusogeza Kombe la Dunia 2022.
“Shirikisho la soka la Afrika limekubaliana na hilo na halitaandaa Kombe la Afrika mwezi Januari mwaka 2023,” alisema Valcke.
“Watapaswa kuahirisha Kombe la Mataifa Afrika hadi Juni.”
Kombe la Dunia 2022 limepangwa kumalizika mwishoni mwa Disemba na Kombe la Afrika limepangwa kuanza kati kati ya Januari 2023.
Valcke alisema lengo la kuahirisha tukio hilo la bara lilikuwa “kuepuka kuachiwa kwa wachezaji wa Afrika kwenye vilabu vyao kwa ajili ya Kombe la Dunia na tena baada ya wiki mbili baada ya Kombe la Mataifa ya Afrika.
0 comments:
Post a Comment