Mbwa mmoja wa Polisi huko New Jersey Marekani mwenye umri wa miaka nane aliyefanya kazi kwa miaka minne amelazimika kustaafu kutokana na afya yake kuwa mbaya.
Mbwa huyo wa Polisi ambaye anaitwa Judge amepewa heshima na kuagwa kishujaa, kwa kuandaliwa gwaride pamoja na kupigiwa saluti na Polisi,tukio hilo pia lilishuhudiwa na watu wa haki za wanyama.
Judge alitakiwa kustaafu kama mbwa wa Polisi katika kituo cha West Deptford, New Jersey tangu mwaka 2013, kutokana na maradhi ya meno na pia afya yake kuwa sio nzuri.
Watu wa haki za wanyama walishauri mbwa huyo ‘astaafishwe’ na pia apelekwe kupatiwa matibabu katika Hospitali ya wanyama ya Swedesboro.
Tukio hilo sio geni sana kwa wenzetu, ukilinganisha na story iliyomhusu mbwa mmoja wa Polisi ambaye alizikwa kwa heshima kama ambavyo huwa mazishi ya askari yanafanyika.
0 comments:
Post a Comment