Marekani yataka Sudan Kusini kuwekewa vikwazo


Rais wa Sudan Salva Kiir akipeana mkono na kiongozi wa waasi Riek Machar, katikati ni Rais wa Tanzania, Dr. Jakaya Mrisho Kikwete
Rais wa Sudan Salva Kiir akipeana mkono na kiongozi wa waasi Riek Machar, katikati ni Rais wa Tanzania, Dr. Jakaya Mrisho Kikwete
Marekani iliwasilisha mapendekezo kwa Umoja wa Mataifa kuiwekea vikwazo Sudan Kusini ambayo imeshindwa kusitisha vita ya miezi 14.
Hatua hizo zilitumwa kwenye Baraza la Usalama siku moja baada ya Ethiopia kufungua ukurasa wa makubaliano kati ya pande zinazopigana zilizotolewa kama fursa ya mwisho kufikia makubaliano.
Chini ya mapendekezo hayo, Baraza la Usalama linaweza kuweka vikwazo vya kusafiri duniani na kupiga tanji mali za watu wanaohatarisha utulivu wa Sudan Kusini.
Pendekezo hilo linaweza kuweka vikwazo vya silaha nchini Sudan Kusini, hatua inayoungwa mkono na nchi za Ulaya pamoja na kwamba adhabu hiyo inaweza kuviadhibu vikosi vya Rais Salva Kiir zaidi ya wapiganaji wa muasi Riek Machar.
“Viongozi wa siasa wameshindwa kuweka ajenda zao za siasa na uchumi pembeni ili kutafuta suluhisho la kisiasa ambalo litaweza kuleta utulivu,” alisema afisa wa Marekani.
Share on Google Plus

About nellychazzy

I Run And Own Nellychazy.blogspot.com. Working With Web Editing, Blogs Template Fix And Editing (HTML). Monitoring click4hosting.net Deals with Web hosting. Also Base On Software And Hardware, Phones,Computer
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Blogger Tricks