Cannavaro kukosa mchezo wa Kombe la Shirikisho Afrika
Cannavaro amesema amejiondoa kwenye kikosi hicho baada ya kupata majeraha juu ya jicho la kushoto na kusababisha kushonwa nyuzi saba.
Nahodha huyo ameongeza kuwa, matibabu ya jicho lake aliyapata siku ya Jumatatu asubuhi kwenye Hospitali ya Kilwa Road, Kurasini jijini Dar es salaam mara baada ya mechi hiyo kumalizika.
Aliongeza kuwa, hataweza kucheza kutokana na maumivu makali anayoyasikia kwenye jeraha hilo, hivyo ameona ni vyema akapumzika hadi jeraha hilo litakapopona kabisa kwa hofu ya kujitonesha.
“Ninatamani kucheza mechi na Platnum, lakini kutokana na jeraha hili kiukweli sitaweza kucheza maana nina hofu kijitonesha”.
0 comments:
Post a Comment