Cannavaro kukosa mchezo wa Kombe la Shirikisho Afrika

Cannavaro akiwa na baadhi ya wauguzi mara baada ya kushonwa nyuzi
Cannavaro akiwa na baadhi ya wauguzi mara baada ya kushonwa nyuzi
Beki mahiri wa kati wa Yanga, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, amejiondoa kwenye kikosi hicho kitakachopambana na Platinum ya Zimbabwe katika mchezo wa kombe la shirikisho Afrika ambao utafanyika wikiendi hii kwenye uwanja wa taifa.
Cannavaro amesema amejiondoa kwenye kikosi hicho baada ya kupata majeraha juu ya jicho la kushoto na kusababisha kushonwa nyuzi saba.
Nahodha huyo ameongeza kuwa, matibabu ya jicho lake aliyapata siku ya Jumatatu asubuhi kwenye Hospitali ya Kilwa Road, Kurasini jijini Dar es salaam mara baada ya mechi hiyo kumalizika.
Aliongeza kuwa, hataweza kucheza kutokana na maumivu makali anayoyasikia kwenye jeraha hilo, hivyo ameona ni vyema akapumzika hadi jeraha hilo litakapopona kabisa kwa hofu ya kujitonesha.
“Ninatamani kucheza mechi na Platnum, lakini kutokana na jeraha hili kiukweli sitaweza kucheza maana nina hofu kijitonesha”.
Share on Google Plus

About nellychazzy

I Run And Own Nellychazy.blogspot.com. Working With Web Editing, Blogs Template Fix And Editing (HTML). Monitoring click4hosting.net Deals with Web hosting. Also Base On Software And Hardware, Phones,Computer
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Blogger Tricks