Leo ni Jumamosi tarehe 23 Mfunguo Nane Jamad al-Awwal 1436 Hijria ambayo inasadifiana na tarehe 14 Machi mwaka 2015 Miladia.
Siku
kama ya leo miaka 37 iliyopita yaani tatrehe 14 Machi 1978, jeshi la
utawala wa Kizayuni wa Israel lilianza kuivamia na kuikalia kwa mabavu
ardhi ya Lebanon kwa kisingizio cha kukabiliana na operesheni
iliyofanywa na wanamapambano wa Kipalestina pambizoni mwa Tel Aviv.
Katika mashambulio hayo jeshi la Israel liliua raia wengi wasio na hatia
wa Lebanon na Palestina na kuikalia kwa mabavu sehemu ya ardhi ya
Lebanon. Hata hivyo utawala huo ghasibu uliondoka kwa fedheha katika
maeneo ya kusini mwa Lebanon mwaka 2000 baada ya kupata kipigo kikali
kutoka kwa wanamapambano shupavu wa Harakati ya mapambano ya Kiislamu ya
Hizbullah na kuondoka kwenye eneo hilo.***
Katika siku kama ya leo
miaka 136 iliyopita, alizaliwa nchini Ujerumani Albert Einstein, msomi
mashuhuri wa fizikia na hisabati. Mnamo mwaka 1921 msomi huyo mahiri
alipewa tuzo ya Nobel katika taaluma ya fizikia, baada ya kufanya juhudi
kubwa za kiutafiti. Utafiti na nadharia za Einstein katika uwanja wa
nyuklia zilikuwa na taathira kubwa duniani. Hata hivyo Einstein
alisikitika sana baada ya kugundua kwamba, uchunguzi na utafiti wake
umetumiwa na baadhi ya nchi kwa ajili ya kutengeneza silaha hatari za
nyuklia. Albert Einstein alifariki dunia mwaka 1955. ***
Na miaka 129
iliyopita katika siku kama ya leo kulingana na kalenda ya Hijria,
aliaga dunia Sayyid Muhammad Ibrahim mashuhuri kwa lakabu ya Sayyidul
Ulamaa, alimu na fakihi wa Kiislamu wa nchini India. Alikuwa mmoja wa
maulama watajika na mahiri mwanzoni mwa karne ya 14 Hijria. Baada ya
kufariki dunia baba yake, Muhammad Ibrahim alichukua jukumu la baba yake
la kueneza mafundisho ya dini katika baadhi ya miji ya India.
Mwanazuoni huyo alifanya hima kubwa ya kueneza misingi na itikadi za
Kiislamu katika ardhi ya India
- Blogger Comment
- Facebook Comment
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)
0 comments:
Post a Comment