Msanii ambaye anafanya bongo fleva kutoka Sweeden Saraha ambaye kawa
sasa yupo hapa bongo kwa mara ya kwanza kabisa tangu kuvunjika kwa
mahusiano yake na mtayarishaji muziki maarufu Fundi Samweli,
Fundi Samweli na Saraha enzi za penzi lao
kupitia mahojiano yake na eNewz ameeleza kuwa mapenzi sio suala
rahisi, na kusisitiza kuwa hakuna shida yoyote kubwa iliyosababisha
kutengana kwao.
Saraha ameieleza eNewz kuwa, safari yao ya mahusiano ilifikia mahali
ambapo kila mmoja aliona kuna umuhimu wa kuchukua njia yake tofauti,
huku akisisitiza kuwa kwa sasa, mpenzi wake mkubwa ni muziki tu ambao
yupo nao wakati wote.
Saraha amesema kuwa, anajipanga kwaajili ya kurejea nchini ndani ua
miezi kadhaa kwaajili ya upigaji picha za video yake mpya katika
kuthibitishia mashabiki kuwa muziki, hususan ule wa Bongo Flava ndio
mpenzi wake mkubwa sasa.
- Blogger Comment
- Facebook Comment
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)
0 comments:
Post a Comment