Saraha afunguka kuvunjika kwa uhusiano wake na Fundi Samweli

Msanii ambaye anafanya bongo fleva kutoka Sweeden Saraha ambaye kawa sasa yupo hapa bongo kwa mara ya kwanza kabisa tangu kuvunjika kwa mahusiano yake na mtayarishaji muziki maarufu Fundi Samweli,
IMG_0230
Fundi Samweli na Saraha enzi za penzi lao
kupitia mahojiano yake na eNewz ameeleza kuwa mapenzi sio suala rahisi, na kusisitiza kuwa hakuna shida yoyote kubwa iliyosababisha kutengana kwao.
Saraha ameieleza eNewz kuwa, safari yao ya mahusiano ilifikia mahali ambapo kila mmoja aliona kuna umuhimu wa kuchukua njia yake tofauti, huku akisisitiza kuwa kwa sasa, mpenzi wake mkubwa ni muziki tu ambao yupo nao wakati wote.
Saraha amesema kuwa, anajipanga kwaajili ya kurejea nchini ndani ua miezi kadhaa kwaajili ya upigaji picha za video yake mpya katika kuthibitishia mashabiki kuwa muziki, hususan ule wa Bongo Flava ndio mpenzi wake mkubwa sasa.
Share on Google Plus

About nellychazzy

I Run And Own Nellychazy.blogspot.com. Working With Web Editing, Blogs Template Fix And Editing (HTML). Monitoring click4hosting.net Deals with Web hosting. Also Base On Software And Hardware, Phones,Computer
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Blogger Tricks