Ufisadi mwingine wa zaidi ya Sh252 bilioni umeibuliwa na Mdhibiti na
Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Profesa Mussa Assad ndani ya
Wizara ya Ujenzi.
Ukaguzi maalumu uliofanywa na ofisi ya (CAG) katika kipindi cha mwaka
wa fedha 2010/11 na 2011/12 umebaini kuwa taarifa iliyotolewa na Waziri
wa Ujenzi, Dk John Magufuli, bungeni Novemba 2013 kuwa fedha hizo
zilitumika kwa miradi ya ujenzi wa barabara, haikuwa sahihi.
Kutokana na ufisadi huo, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za
Serikali (CAG) amependekeza hatua stahiki zichukuliwe kwa wahusika wa
Wizara ya Ujenzi na wakala wa barabara ili kuleta imani na uwazi kwa
jamii na wahisani kuhusu bajeti ya nchi.
- Blogger Comment
- Facebook Comment
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)

0 comments:
Post a Comment