Msanii wa muziki wa kizazi kipya, Young Killer, amesema ana ndoto za kufikia mafanikio aliyonayo mwanamuziki wa kimataifa, Jay Z.
Akizungumza na Mwandishi jijini Dar es Salaam, Killer, alisema dhamira yake ni kuwa msanii mkubwa kama huyo wa Marekani.
“Natamani siku moja nifikie uwezo na mafanikio kama ya Jay Z, nampenda sana,” alisema Killer.
Alisema ili kufikia hatua hiyo, atafanya bidii kuhakikisha anapata mafanikio makubwa.
“Hizo ndizo ndoto zangu za kusonga mbele zaidi, napenda kuiga anayofanya nguli huyo wa Marekani,” alisema msanii huyo.
0 comments:
Post a Comment