Zidane ajipanga kuiongoza timu ya taifa ya Ufaransa


Zinedine Zidane
Zinedine Zidane
Mshambuliaji wa zamani wa klabu ya Real Madrid na timu ya taifa ya Ufaransa Zinedine Zidane amesema kuwa ana matarajio ya kuiongoza timu ya taifa ya Ufaransa kwa siku za mbeleni.
Hata hivyo Zidane ameongeza kuwa endapo hatakuwa kocha mkuu wa timu hiyo basi ataangalia mambo mengine ambayo anaweza kufanya ndani ya kikosi hicho.
Wakati Zidane anaongea na chombo cha habari cha Canal+Francia alisema kuwa” nadhani mmenielewa, malengo na matarajio yangu nikuwa kocha wa timu ya Ufaransa lakini sijuhi ni lini na siku gani maana bado nina muda wa kusonga mbele”.alisema Zinedine.
Nyota huyo enzi za uchezaji wake aliweza kunyakuwa makombe mbalimbali kama,kombe la dunia, kombe la mabingwa ulaya pamoja na medali nyingi na kwasasa ni kocha wa kikosi cha akiba cha wachezaji wa klabu ya Real Madrid.
Share on Google Plus

About nellychazzy

I Run And Own Nellychazy.blogspot.com. Working With Web Editing, Blogs Template Fix And Editing (HTML). Monitoring click4hosting.net Deals with Web hosting. Also Base On Software And Hardware, Phones,Computer
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Blogger Tricks