Referee ajikuta akishangilia goli la Tottenham

Referee ajikuta akishangilia goli la Tottenham.
Referee ajikuta akishangilia goli la Tottenham.
Baada ya mchezo wa jana kati ya Tottenham dhidi ya Aston Villa uliochezwa kwenye uwanja wa White Hart Lane, kumeibuka mijadala kwenye mitandao ya kijamii ambapo baadhi ya watu wamemtuhumu mwamuzi Mike Dean aliyechezesha mchezo huo kuwa alishangilia goli la kwanza lililofungwa na Mousa Dembele.

Referee, Mike Dean, alionekana kama akishangilia bao alilofunga Dembele kutoka na ishara za mikono yake.
Referee, Mike Dean, alionekana kama akishangilia bao alilofunga Dembele kutoka na ishara za mikono yake.
Dean alimpa ‘advantage’ Dembele kabla ya kufunga goli hilo ambalo lilikuwa la kwanza kwa Tottenham, Dean alionekana kwenye picha za video kama anashangilia goli hilo.
Mike Dean
Mike Dean
Madai hayo yameunganishwa na matukio ya nyuma ya mwamuzi huyo yanayoihusu Tottenham ambapo mara kadhaa ameonekana akichukizwa endapo amempa advantage mchezaji wa timu hiyo halafu akapoteza mpira lakini mara kadhaa amekuwa akihusishwa kuipendelea timu hiyo na mara nyingine kushangilia magoli yanayofungwa na Tottenham.
Lakini baadhi ya wadau wa soka wanadai kuwa mwamuzi huyo amekuwa akifurahishwa na matukio mazuri uwanjani bila kujali timu gani imefanya tukio ambalo limemvutia Dean.
January 2014 wakati Manchester United inacheza mchezo wa FA Cup dhidi ya Swansea City kwenye uwanja wa Old Trafford, Dean alionekana kutoridhishwa na Swansea kushindwa kutumia vyema advantage aliyowapa.
Lakini mwaka 2012 inadaiwa Dean alishindwa kujizuia na akajikuta akishangilia goli la Luis Saha lilofungwa kwenye mchezo wa London Derby kati ya Arsenal dhidi ya Tottenham.
Share on Google Plus

About nellychazzy

I Run And Own Nellychazy.blogspot.com. Working With Web Editing, Blogs Template Fix And Editing (HTML). Monitoring click4hosting.net Deals with Web hosting. Also Base On Software And Hardware, Phones,Computer
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Blogger Tricks