Nahodha wa Arsenal Thomas Vermaelen amekubali dau la kujiunga na Manchester United msimu huu wa jua.
United lazima wakubali ada ya Arsenal baada ya Kombe la Dunia, ila Vermaelen ana matumaini ya kuhamia Old Trafford na anajiandaa kuondoka Emirates.
Mlinzi huyo wa kati Varmaelen ana mwaka mmoja pekee uliobaki kwenye mkataba wake Arsenal na amejiona mwenyewe akitolewa kwenye kikosi cha kwanza cha Arsene Wenger anayewapanga Laurent Koscielny na Per Mertesacker.
Kocha mpya wa United Louis van Gaal ana hasira ya kuiimaarisha safu ya ulinzi ya United na anaamini Vermaelen anaweza kufanya vizuri akiwa naye.
Vermaelen, 28, amekuwa Arsenal kwa miaka mitano baada kusaini akitokea klabu ya Uholanzi ya Ajax. Alianza vizuri akiwa na Washika bunduki, ila majeraha yakazuia maendeleo yake.
0 comments:
Post a Comment