Oscar Pistorius afutiwa shtaka la kuua

Oscar Pistorius akiwa amekaa huku akisikiliza hukumu iliyokuwa inayotolewa na Jaji Thokozile Masipa.
Oscar Pistorius akiwa amekaa huku akisikiliza hukumu iliyokuwa inatolewa na Jaji Thokozile Masipa.
Jaji wa kesi ya Oscar Pistorius ametupilia mbali hukumu ya mauaji ya kukusudia, na kusema mashtaka yalishindwa kuthibitisha kuwa (Oscar) alimuua mpenzi wake kwa kukusudia baada ya malumbano...>>>>

Ila Jaji Thokozile Masipa pia alikataa hoja za walalamikaji kwamba mwanariadha huyo alikosa uwezo wa kujizuia kufanya uhalifu.
Jaji alisema aliridhishwa na mshtakiwa “kuweza kutofautisha kati ya baya na zuri,” alisema alikuwa shuhuda aliyejaribu kuepuka ila haimanishi alikuwa mkosaji.
Oscar Pistorius akiwa na mpenzi wake Reeva Steenkamp Novemba 2012 mjini Johannesburg, miezi mitatu kabla hajamuua.
Oscar Pistorius akiwa na mpenzi wake Reeva Steenkamp Novemba 2012 mjini Johannesburg, miezi mitatu kabla hajamuua.
Mwanariadha huyo wa Olimpiki wa Afrika Kusini anakataa kumuua Bi Steenkamp siku ya Valentine mwaka uliopita, akisema alifikiri ni jambazi.
Oscar Pistorius atakabiliwa na hukumu ya kifungo cha muda mrefu jela endapo Jaji atamkuta na kosa la kuua kwa bahati mbaya.
Share on Google Plus

About nellychazzy

I Run And Own Nellychazy.blogspot.com. Working With Web Editing, Blogs Template Fix And Editing (HTML). Monitoring click4hosting.net Deals with Web hosting. Also Base On Software And Hardware, Phones,Computer
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Blogger Tricks