Mamlaka ya uhamiaji nchini Uganda ilimtia mbaroni mwanamuziki Desire Luzinda kwa kosa la kutumia pesa kinyume na makubaliano na mkopeshaji wake.
Inasemekana msanii huyo baada ya kuchukua zile pesa alizitumia kumsaidia mpenzi wake raia wa Nigeria ili kuchukua passport ya Uganda.
Desire alitiwa mbaroni kwenye uwanja wa kimataifa wa Entebbe siku ya Jumamosi asubuhi wakati akirejea kutoka kwenye tamasha nchini Congo Brazzaville.
Msemaji wa polisi Bw. Fred Enanga alithibitisha kukamatwa kwa msanii huyo.
0 comments:
Post a Comment