Klabu ya Manchester United imeanza mazungumzo na wakala wa mchezaji Christiano Ronaldo kwa lengo la kumrudisha katika klabu yake hiyo ya zamani ya Old Trafford.
Kumekuwa na uvumi kuwa mchezaji huyo haridhishwi na maisha anayoishi katika klabu yake ya sasa ya Real Madrid na huenda safari yake ya kurudi Manchester United ikawa kweli baada ya viongozi wa timu hiyo kuanza mazungunzo na bosi wake Jorge Mendes.
Kwa mujibu wa gazeti la Metro la Uingereza, United ina matumaini ya kumpata Ronaldo kwa kitita cha Euro millioni 100 ambazo ni sawa na pauni millioni 71.1. huku hakika wa raia huyo wa Ureno kukubali kurudi Manchester United upo juu yake.
0 comments:
Post a Comment