Watanzania wawili wauawa Afrika Kusini


Ghasia za kuwashambulia wageni zilizoanza Durban wiki mbili zilizopita zimesababisha vifo vya Watanzania wawili
Ghasia za kuwashambulia wageni zilizoanza Durban wiki mbili zilizopita zimesababisha vifo vya Watanzania wawili
Watanzania wawili wanaoishi Afrika Kusini wameuawa kwa kile kinachohusisha muendelezo wa hofu na chuki dhidi ya wageni ambao umetikisa hivi karibuni.
Taarifa ya vifo imekuja baada ya Waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa Mhe. Bernard Membe, kutangaza kutoka Oman kwamba Tanzania imeanza kuondoa raia wake kutoka Yemen ambapo kumekumbwa na vita ya umwagaji damu baina ya majeshi ya serikali na waasi.
Wageni wakiwa na silaha za jadi tayari kupamba na wenyeji waliokuwa wakivamia maduka yao mjini Durban
Wageni wakiwa na silaha za jadi tayari kupamba na wenyeji waliokuwa wakivamia maduka yao mjini Durban
Nchini Afrika Kusini, mwakilishi wa Watanzani waishio nchini humo aliiambia The Citizen jana, kwamba watu wawili wameuawa katika ghasia za kushambulia wageni ambazo zimesababisha vifo vya watu watano kutoka mataifa mengine na kuwakoseasha makazi maelfu katika mji wa Durban.
Bw Bonka Kusekela, mwakilishi wa Watanzania, alitaja majina ya marehemu kama Rashid Jumanne, muuza sigara ambaye aliuawa Jumanne huko Stenga, mtaa uliopo Durban na mwingine ni Athumani maarufu kama China Mapepe, ambaye aliuawa Jumanne katika jiji kubwa la jimbo la KwaZulu-Natal nchini Afrika Kusini.
Jamaa akiwa na panga huku akishangiliwa na wenzake mjini Johannesburg
Jamaa akiwa na panga huku akishangiliwa na wenzake mjini Johannesburg
Kwa mujibu wa Kusekela, Rashid alipigwa risasi na mtu asiyejulikana wakati akifanya biashara yake wakati Athumani, mfungwa katika gereza kurekebisha makosa la Westville alichoma kisu hadi kufa na wafungwa wenzake.
“Ninavyozungumza nanyi sasa tuko katika maandamano ya amani na baadhi ya wenyeji mjini Durban kulaani mauaji haya ya kikatili lakini tumeshapoteza Watanzania wawili mpaka sasa,” aliiambia The Citizen kwa simu kutokea Durban.
Mtuu mmoja akiwa ameshika jiwe kufuatia ghasia hizo ambazo zimesababisha vifo vya watu watano
Mtuu mmoja akiwa ameshika jiwe kufuatia ghasia hizo ambazo zimesababisha vifo vya watu watano
Lakini kwa majibu ya haraka, Balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini Elibariki Ngoyai Lowassa alisema hakuna taarifa rasmi kwamba watu wawili wamefariki kutokana muendelezo wa ghasia dhidi ya wageni.
Akizungumza na The Citizen kutoka Afrika Kusini, hatahivyo, Bw Lowassa, alithibitisha vifo vya Watanzania wawili.
Polisi wa Afrika Kusini wakitumia risasi za plastiki kutawanya magenge ya wahamiaji waliokuwa wakipambana nao
Polisi wa Afrika Kusini wakitumia risasi za plastiki kutawanya magenge ya wahamiaji waliokuwa wakipambana nao
Chanzo: The Citizen
Share on Google Plus

About nellychazzy

I Run And Own Nellychazy.blogspot.com. Working With Web Editing, Blogs Template Fix And Editing (HTML). Monitoring click4hosting.net Deals with Web hosting. Also Base On Software And Hardware, Phones,Computer
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Blogger Tricks