MIDA YA WANGA 1


...nililitizama lile sufuria huku mate yakinidondoka.Nilikuwa sina budi kuuchochea moto baada ya kukata kata zile nyama za wale watoto kumi tuliokuwa tumewatoa kwenye hospitali teule ya Uswazi.
Macho na vidole vyote vya wale watoto nilikuwa nimeisha vila na kujiridhisha kuwa nyama ya siku hiyo ilikuwa murua. Kuwapata watoto wale haikuwa kazi ngumu kwani mkuu wa kilinge chetu Hamza ndiyo alikuwa mkuu wa kitendo cha wajawazito katika hospitali hiyo. Muda wote huu shamra shamra za hapa na pale zilikuwa bado zikiendelea na zile aibu za mara ya kwanza za kucheza uchi wote walikuwa wamezifukia kwenye kaburi la sahau na sasa sherehe ilikuwa imepamba moto.Sherehe kama hizi huwa tunazifanya kila mwisho wa mwaka kujipongeza kwa kazi nzuri tulizofanya mwaka mzima.Nililifungua lile sufuria kwa mara nyingine na kutoka na kipande cha mkono nika.............

Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Blogger Tricks