Ombi kwa facebook dhidi ya binti mdogo aliyeua chui na wanyama wengine wakali.

bintichui
Baadhi ya watumiaji wa mtandao wa Facebook wameanzisha kampeni kubwa kuitaka kampuni hiyo kuondoa picha za binti mdogo mwindaji anayeonekana amepiga picha na wanyama wakali anaodai kuwaua katika nchi za kiafrika ikiwemo Zimbabwe...>>

Binti huyo Kendall Jones kutoka Cleburne, Texas, anadaiwa kuwa ni mwindaji mdogo zaidi kuwapiga risasi wanyama hao wakali wa mwituni akiwemo Chui na kuthibitisha hilo amekuwa akipozi nao kwa picha baada ya kufanya kitendo hicho.
bintichui2

Maelfu ya watu wanaitaka Facebook kuondoa picha hizo ambapo binti huyo amejitetea kuwa anafurahi kuendeleza ndoto zake.
bintichui3Lakini pia binti huyo ameandika kupitia akaunti yake ya Facebook kuwa anatarajia kuanzisha kipindi chake cha Televisheni ifikapo mwaka 2015.
Binti huyo amekuwa akitabasamu na kuweka pozi pembeni ya wanyama wa aina mbalimbali anaodai kuwaua ambapo picha hizo zimeamsha hisia kali katika mitandao ya kijamii watu wakidai ziondolewa.
Share on Google Plus

About nellychazzy

I Run And Own Nellychazy.blogspot.com. Working With Web Editing, Blogs Template Fix And Editing (HTML). Monitoring click4hosting.net Deals with Web hosting. Also Base On Software And Hardware, Phones,Computer
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

Blogger Tricks